Consesar Mark Massawe
Organization University of Eastern Finland
Pays Tanzanie
Région
Secteur Conseil / prestataire de services
Poste / titre du poste Researcher
My experience in adult learning and education
Elimu ya watu wazima ni utaratibu wa kufundisha na kuwashirikisha watu wazima katika shughuli za kujifunza. Utaraibu huu ni wa hiari na lengo lake ni kupata maarifa, ujuzi, mitazamo, au maadili mapya. Mpango huu wa elimu ya watu wazima inawahusu zaidi watu waliopitisha umri wa kwenda shule kwa lazima. Inalenga kufundisha maisha yote kwa ajili ya maendeleo ya kazi, kujiongezea maarifa, kusoma na kuandika. Mpango huu umewekwa katika mifumu mengi ili kuruhusu watu kutoka kwenye matabaka mbali mbali kuhudhuria. Nimeshafanya kazi ya kuwaongoza na kuwasaidia watu wazima kusoma na kufanya mitihani ya secondary na kuweza kufika mpaka chuo kikuu kule Tanzania. Miongoni mwa hao wengi wana kazi nzuri na wamebadilisha maisha yao na ndugu zao.